Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali
Angawa mdogo, dagaa, amekomaa
Kaanga kidogo, dagaa,atakufaa
Kalia kinaya,dagaa h’ondoa njaa
Wa kwako udogo, kijana, sio balaa
Na sio mzigo, kijana bado wafaa
Toka kwa mtego, kijana sinyanyapaa
Nasaha kidogo, kijana, ukubwa jaa
Jikaze kimbogo, kijana, acha kukaa
Chimbua mhogo, kijana, usibung’aa
Na wake udogo,dagaa, ndani hukaa,
Kuliko vigogo, dagaa, hujambaa
Hapati kipigo,dagaa hana fazaa
Maisha si mwigo, kijana, ushike taa
Sihofu magego, kijana, nawe wafaa
Kazana kidogo, kijana, kugaagaa
MASWALI
a) Lipe shairi hili anwani mwafaka (al 2)
b) Eleza arudhi zilizofuatwa katika kutunga shairi hili (al 4)
c) Onyesha jinsi malenga alivyotumia uhuru wake (al 3)
d) Tambua bahari katika shairi hili (al 3)
e) Andika ubeti wa tatu kwa lugha ya nathari (al 4)
f) Tambua mbinu za lugha zilizotumika katika shairi (al 2)
g) Eleza toni ya shairi hili (al 2)
MAJIBU
Oops! Unlock More Access Rights:
If you find that you are not subscribed, consider upgrading your account or subscribing to the necessary plan to gain access.
Discover more from ELIMU ASSISTANT
Subscribe to get the latest posts sent to your email.
