Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali

 Angawa mdogo, dagaa, amekomaa

Kaanga kidogo, dagaa,atakufaa

Kalia kinaya,dagaa h’ondoa njaa

 

Wa kwako udogo, kijana, sio balaa

Na sio mzigo, kijana bado wafaa

Toka kwa mtego, kijana sinyanyapaa

 

Nasaha kidogo, kijana, ukubwa jaa

Jikaze kimbogo, kijana, acha kukaa

Chimbua mhogo, kijana, usibung’aa

 

Na wake udogo,dagaa, ndani hukaa,

Kuliko vigogo, dagaa, hujambaa

Hapati kipigo,dagaa hana fazaa

 

Maisha si mwigo, kijana, ushike taa

Sihofu magego, kijana, nawe wafaa

Kazana kidogo, kijana, kugaagaa

 

MASWALI

a) Lipe shairi hili anwani mwafaka (al 2)
b) Eleza arudhi zilizofuatwa katika kutunga shairi hili (al 4)
c) Onyesha jinsi malenga alivyotumia uhuru wake (al 3)
d) Tambua bahari katika shairi hili (al 3)
e) Andika ubeti wa tatu kwa lugha ya nathari (al 4)
f) Tambua mbinu za lugha zilizotumika katika shairi (al 2)
g) Eleza toni ya shairi hili (al 2)

MAJIBU

Upgrade or Subscribe

Oops! Unlock More Access Rights:

If you find that you are not subscribed, consider upgrading your account or subscribing to the necessary plan to gain access.


Discover more from ELIMU ASSISTANT

Subscribe to get the latest posts sent to your email.

Elimu Assistant Team

By Elimu Assistant Team

Get in Touch! Need educational resources? Reach out! I'm here to help. Name: Mr. Atika Email: nyamotima@yahoo.com Phone: 0728450425 (Safaricom) | 0738619279 (Airtel)

Leave a Reply

Discover more from ELIMU ASSISTANT

Subscribe now to keep reading and get access to the full archive.

Continue reading